Mkuu wa Wilaya Ludewa ashiriki uzinduzi wa kiwanda cha Itracom Dodoma | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kilimo

Mkuu wa Wilaya Ludewa ashiriki uzinduzi wa kiwanda cha Itracom Dodoma

Mkuu wa Wilaya ya Ludewa ni miongoni mwa viongozi waliopokea maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia Dk Samia Suluhu Hassan ya kutaka kuenda kusimamia Sekta ya kilimo ipasavyo katika maeneo yao.

The Dododma Post
By The Dododma Post
28 Jun 2025
Mkuu wa Wilaya Ludewa ashiriki uzinduzi wa kiwanda cha Itracom Dodoma

Rais Samia ameagiza Kiwanda cha Mbolea cha Intracom cha jijini Dodoma kuimarisha mfumo ya usambazaji wa mbolea hadi vijiji ili kuwawezesha  wakulima kupata mbolea kwa gharama ndogo.
Rais Samia ameyasema hayo Juni 28,2025 wakati akizindua Kiwanda cha Mbolea cha Intracom cha jijini Dodoma.
Amesema kikwazo kikubwa ni upatikanaji wa mbolea pamoja na gharama zake, hivyo Serikali wamejipanga kutoa ruzuku za mbolea na wanatoa na sasa wanapata mbolea.
“Sekta hii ni muhimu, Serikali tuko tayari kumfanya mkulima kuzalisha kwa tija ili Serikali iweze kuuza nje kwa bei yenye tija,”amesema.
Amesema kuwa kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Kimataifa itakapofika mwaka 2050 nchi takribani 26 zitakuwa na ongezeko la kwa asilimia 100 ya waliokuwa nao 2015, hivyo upatikanaji wa chakula ni muhimu. 
Amesema soko la mbolea bado liko kubwa nchini na kikubwa ni kuwa uzalishaji wa mbolea katika kiwanda hicho unatumia maligjhafi zilizokuwa nchini, hivyo ni mnyororo wa kuongeza thamani kutoka kwa mkulima.

SERIKALI IMEPUNGUZA TOZO KATIKA ZAO LA KAHAWA KUTOKA 17 HADI 5.

SERIKALI IMEPUNGUZA TOZO KATIKA ZAO LA KAHAWA KUTOKA 17 HADI 5.

RAIS SAMIA AWAAGIZA WAKUU WA MIKOA KUSIMAMIA KILIMO

RAIS SAMIA AWAAGIZA WAKUU WA MIKOA KUSIMAMIA KILIMO

UZALISHAJI WA MBEGU BORA NDANI YA NCHI UMEONGOZEKA

UZALISHAJI WA MBEGU BORA NDANI YA NCHI UMEONGOZEKA

RAIS SAMIA Ameziagiza Wizara ya Fedha,Kilimo Kukaa pamoja na BOT Kuja na Sera ya Taifa.

RAIS SAMIA Ameziagiza Wizara ya Fedha,Kilimo Kukaa pamoja na BOT Kuja na Sera ya Taifa.

SEKTA Ya Kilimo Inakabiliwa na Changamoto ya Kupanda kwa Bei ya Mbolea

SEKTA Ya Kilimo Inakabiliwa na Changamoto ya Kupanda kwa Bei ya Mbolea