UDOM KUJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA KUUZA VIMIMINIKA. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

UDOM KUJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA KUUZA VIMIMINIKA.

Chuo kikuu Dodoma UDOM kimekuja na teknolojia mpya ya uuzaji wa vimiminika kidigital ambapo imekuja kutatua changamoto mbalimbali za wajasiliamali lakini pia kuokoa muda.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
03 Jul 2025
UDOM KUJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA KUUZA VIMIMINIKA.

Chuo kikuu Dodoma (UDOM) kimekuja na teknolojia mpya ya uuzaji wa vimiminika kidigital ambapo imekuja kutatua changamoto mbalimbali za wajasiliamali lakini pia kuokoa muda.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 49 ya biashara Sabasaba jijini Dar es salaam julai 3,2025 muhazili Mwandamizi kwenye ndaki ya sayansi za komputa na elimu angavu kutoa UDOM Hassan kilavo amesema kufuatia kasi ya ukuaji wa teknolojia ndio umepelekea chuo hiko kubuni mashine hiyo ya kuuzia vimiminika.

"Hii ni teknolojia ni mpya hapa kwetu tumeianzisha mahususi kwa ajili ya wafanyabiashara wa vimiminika kwani kwa kutumia mashine hii utaweza kuokoa muda na haiitaji muhudumu kwani inaweza kusetiwa na mtu akajihudumia mwenyewe",amesema

Aidha amesema mashine hiyo inatoa huduma ya kidigital kwani inamifumo ya malipo ya kidigital ambapo haiitaji mtu kuwepo ili kupata huduma badala yake mteja anaweza kujihudumia mwenyewe

Sambamba ameongeza kuwa ikiwa mjasiliamali anamtaji wake lakini hana mashine wanaweza kuingia makubalino na kumpatia mashine kwa mkopo au kwa maelewano maalumu.

Amesema kama mtu hana milioni 14 ya kununulia wanaweza kukaa chini na kuongea waone namna ambavyo wanaweza kuweka mikakati ya kulipia mashine hiyo.

“Niwaambie wajasiliamali Sasa hivi tunaenda kiteknolojia zaidi kwa hiyo watu watumie keknolojia kwa ajili ya kurahisisha mambo wanayoyafanya”,Amesema.

Mashine hiyo yakuuzia vimiminika imetengenezwa na chuo kikuu Cha UDOM ambapo  zinatengenezwa kutokana na uhitaji wa mtu na aina ya vimiminika vinavyotarajiwa kuuzwa.

SHERIA ZILIZOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA MWEZI AGOSTI.

SHERIA ZILIZOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA MWEZI AGOSTI.

WAZIRI KIKWETE AIPONGEZA OFISI YA MSAJILI WA HAZINA.

WAZIRI KIKWETE AIPONGEZA OFISI YA MSAJILI WA HAZINA.

NISHATI SAFI YA KUPIKIA NI AJENDA YA DUNIA, WIZARA INAITEKELEZA KWA VITENDO - DKT. KAZUNGU.

NISHATI SAFI YA KUPIKIA NI AJENDA YA DUNIA, WIZARA INAITEKELEZA KWA VITENDO - DKT. KAZUNGU.

UKUAJI WA UCHUMI WA TANZANIA BARA UNAKADILIWA KUFIKIA ASILIMIA 5.8:BoT.

UKUAJI WA UCHUMI WA TANZANIA BARA UNAKADILIWA KUFIKIA ASILIMIA 5.8:BoT.

DIB YAHIMIZA WANANCHI KUDAI FIDIA ZAO KUTOKA BENKI ZILIZOFILISIKA

DIB YAHIMIZA WANANCHI KUDAI FIDIA ZAO KUTOKA BENKI ZILIZOFILISIKA