SERIKALI IMEPUNGUZA TOZO KATIKA ZAO LA KAHAWA KUTOKA 17 HADI 5. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kilimo

SERIKALI IMEPUNGUZA TOZO KATIKA ZAO LA KAHAWA KUTOKA 17 HADI 5.

Serikali imepunguza tozo katika zao la kahawa kutoka idadi ya tozo 17 hadi 5 pamoja na kuhakikisha kahawa inauzwa katika minada rasmi.

Moreen Rojas
By Moreen Rojas
01 Jul 2025
SERIKALI IMEPUNGUZA TOZO KATIKA ZAO LA KAHAWA KUTOKA 17 HADI 5.

Hali hii imesababisha Uzalishaji umeongezeka kutoka tani 53,417 hadi tani 54,203 za maganda kwa mwaka,Bei kwa kilo moja kupanda kutoka Tshs. 1,200 hadi Tshs. 4,200.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Hajjat Fatma Mwasa wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya Serikali ya awamu ya Sita tarehe 01 Julai 2025 Katika ukumbi wa Idara ya habari Maelezo jijini Dodoma.

Aidha Vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu vilivyopewa mikopo ya asilimia 10 isiyo na riba vimeongezeka kutoka 630 hadi 1,370.kiwango cha mikopo iliyotolewa nacho kimeongezeka kutoka Tshs. Bil. 3.23 hadi Tshs. Bil. 9.41.Kupitia mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF), kaya zilizonufaika zimeongezeka kutoka 36,045 hadi 380,035.

Aidha, ruzuku iliyotolewa kwa kaya hizo imeongezeka pia kutoka Tshs. Bil. 16.82 hadi Tshs. Bil. 34.86.Katika mpango wa Mkoa wa kuanzisha mashamba makubwa (block farms) ya kahawa na migomba, vijana 300 wamewezeshwa kuanzisha shamba la kahawa la ekari 300 katika kijiji cha Makongora, Muleba likiwa ni shamba namba moja.Kongani 4 za vijana zimeanzishwa katika Wilaya za Missenyi, Bukoba, Muleba na Kyerwa zilizowezesha vijana 180 kujiajiri na kuajiri wengine.

"Idadi ya biashara rasmi zimeongezeka kutoka 16,376 hadi 25,378 sawa na ongezeko la 55%.Wafanyabiashara wadogo (Machinga) waliotambuliwa katika mfumo rasmi wameongezeka kutoka 1,550 hadi 2,821 sawa na 82% na wamewezeshwa kupata ofisi yao iliyogharimu Tshs. Mil. 35 ambapo Mhe. Rais alichangia Tshs. Mil. 10"

"Wawekezaji katika Mkoa wameongezeka kutoka 175 hadi 275, ambapo Kituo cha Uwekezaji (TIC) kimesajili miradi yenye thamani ya Tshs. Bil. 267.16 inayotoa ajira 11,072."

Aidha Makusanyo yameongezeka kutoka jumla ya Tshs. Bil. 23.6 mwaka 2020/21 hadi Tshs. Bil. 47.2 mwaka 2024/25 kufikia mwezi Mei, 2025 sawa na ongezeko la 100%. ambapo kwa kipindi cha miaka mitano (5) zimekusanywa jumla ya Tshs Bil. 175.8

Aidha ameongeza kuwa Tangu mwaka wa fedha 2024/25 Mkoa umekuwa ukitekeleza miradi ya kimkakati ipatayo 28 kwa kutumia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri zake.  

"Miradi hii itagharimu jumla ya Tshs. Bil. 25.93 na hadi sasa zimeshatengwa katika bajeti (mwaka 2024/25 na 2025/26) jumla ya Tshs. Bil. 11.52 na utekelezaji unaendelea katika hatua mbalimbali"

"Baadhi ya miradi hiyo ni Ujenzi soko la kisasa, Muleba Mjini kwa gharama ya Tshs. Bil. 3 - umefikia 41%, Ujenzi wa shule za michepuo ya kiingereza Katika Wilaya ya Kyerwa Tshs. Bil. 1 iliyofikia 40% na Ngara Tshs. Mil. 530 imefikia 78%, Ujenzi wa ukumbi na maduka ya kisasa Katika Wilaya ya Ngara kwa gharama ya Tshs. Mil. 600  umefikia 35%"

"Ujenzi wa ukumbi na maduka ya  kisasa katika Wilaya ya Karagwe kwa gharama ya Tshs. Bil. 2.2. hatua za awali za utekelezaji, Ujenzi wa soko la kisasa la Bunazi/Missenyi kwa gharama ya Tshs. Bil. 16.5. Hatua za kusaini mikataka ya ujenzi na Mkandarasi"

Sanjari na hayo kuna Miradi ya Kimkakati Katika Manispaa ya Bukoba kama Ujenzi wa stendi kuu ya mabasi na Soko kuu la Bukoba - hatua ya kusaini mkataba,Ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 8.8 kwa kiwango cha lami na ujenzi wa kingo za Mto Kanoni zenye urefu wa kilomita 8 - hatua ya kusaini mkataba,Ujenzi wa Stendi ya Mjini Kati kwa gharama ya Tshs. Bil. 1.356 – sawa na utekelezaji wa 80% pamoja na Ujenzi wa masoko ya Kishenge na Machinjioni bajeti imeidhinishwa – utekelezaji utaanza mwaka 2025/26.

Mkuu wa Wilaya Ludewa ashiriki uzinduzi wa kiwanda cha Itracom Dodoma

Mkuu wa Wilaya Ludewa ashiriki uzinduzi wa kiwanda cha Itracom Dodoma

RAIS SAMIA AWAAGIZA WAKUU WA MIKOA KUSIMAMIA KILIMO

RAIS SAMIA AWAAGIZA WAKUU WA MIKOA KUSIMAMIA KILIMO

UZALISHAJI WA MBEGU BORA NDANI YA NCHI UMEONGOZEKA

UZALISHAJI WA MBEGU BORA NDANI YA NCHI UMEONGOZEKA

RAIS SAMIA Ameziagiza Wizara ya Fedha,Kilimo Kukaa pamoja na BOT Kuja na Sera ya Taifa.

RAIS SAMIA Ameziagiza Wizara ya Fedha,Kilimo Kukaa pamoja na BOT Kuja na Sera ya Taifa.

SEKTA Ya Kilimo Inakabiliwa na Changamoto ya Kupanda kwa Bei ya Mbolea

SEKTA Ya Kilimo Inakabiliwa na Changamoto ya Kupanda kwa Bei ya Mbolea