MKURUGENZI TASAC AWATAKA WANANCHI KUSOMA MASOMO YANAYOHUSU SEKTA YA BAHARI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

MKURUGENZI TASAC AWATAKA WANANCHI KUSOMA MASOMO YANAYOHUSU SEKTA YA BAHARI.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika wakala wa Meli Tanzania (TASAC ) Mohamed Salum ametoa rai kwa wananchi kusoma masomo yanayohusu sekta ya bahari na kupata mafunzo ya kitaalamu kwani bado kuna uhaba wa mabaharia Duniani.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
07 Jul 2025
MKURUGENZI TASAC AWATAKA WANANCHI KUSOMA MASOMO YANAYOHUSU SEKTA YA BAHARI.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika wakala wa  Meli Tanzania (TASAC ) Mohamed Salum ametoa rai kwa  wananchi kusoma masomo yanayohusu sekta ya bahari na kupata mafunzo ya kitaalamu kwani bado kuna uhaba wa  mabaharia  Duniani.

Akizungumza leo, Julai,7 2025 jijini Dar es Salaam kwenye maonesho ya 49 Kimataifa ya Biashara Sabasaba amesema Hadi sasa bado kuna uhaba wa baharia  duniani lakini sekta ya bahari ni biashara na inachangia uchumi na ina  fursa mbalimbali.

Akizungumzia ushiriki wao kama TASAC Kwenye maonesho hayo amesema wapo hapo kutoa elimu lakini pia kuwajukisha watu fursa zilizopo kwenye sekta ya bahari.

Akizungumzia majukumu ya TASAC amesema jukumu kubwa ni kusimamia mambo yanayohusu usalama wa bahari,  meli,  maeneo ya bandari na utekelezaji  wa Mkataba wa Usalama wa Meli na maeneo ya bandari(ISPS Code).

Poa ameongeza kuwa wanajukumu la  kusimamia shughuli za bandari kutoa  vibali  eneo linalofaa  na lisilofaa kwa kujenga  bandari.

"Kazi ya TASAC  ni pamoja na kukagua  vyombo vya usafiri  majini, masuala ya kiusalama bandarini na  kudhibiti uchafuzi wa mazingira majini  unaosababishwa na vyombo vya usafiri majini,"amesema.

REA YAJIZATITI KUFIKISHA LENGO LA TAIFA KWENYE NISHATI SAFI YA KUPIKIA

REA YAJIZATITI KUFIKISHA LENGO LA TAIFA KWENYE NISHATI SAFI YA KUPIKIA

SHERIA ZILIZOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA MWEZI AGOSTI.

SHERIA ZILIZOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA MWEZI AGOSTI.

WAZIRI KIKWETE AIPONGEZA OFISI YA MSAJILI WA HAZINA.

WAZIRI KIKWETE AIPONGEZA OFISI YA MSAJILI WA HAZINA.

NISHATI SAFI YA KUPIKIA NI AJENDA YA DUNIA, WIZARA INAITEKELEZA KWA VITENDO - DKT. KAZUNGU.

NISHATI SAFI YA KUPIKIA NI AJENDA YA DUNIA, WIZARA INAITEKELEZA KWA VITENDO - DKT. KAZUNGU.

UDOM KUJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA KUUZA VIMIMINIKA.

UDOM KUJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA KUUZA VIMIMINIKA.