Watu 36 Wafariki Dunia, Majeruhi 23 Wakimbizwa Hospitali | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

Watu 36 Wafariki Dunia, Majeruhi 23 Wakimbizwa Hospitali

Wakati juhudi za uokoaji na uondoshaji wa miili zikiendelea usiku huu wilayani Same mkoani Kilimanjaro, watu 36 wamethibitishwa kufariki dunia katika ajali mbaya iliyohusisha basi la abiria la kampuni ya Chanel One na basi dogo aina ya Coaster, yaliyogongana uso kwa uso na kuwaka moto.

The Dododma Post
By The Dododma Post
28 Jun 2025
Watu 36 Wafariki Dunia, Majeruhi 23 Wakimbizwa Hospitali

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Kilimanjaro, Jeremiah Mkomagi, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema taarifa zilizopo kwa sasa ni za awali huku juhudi za uokoaji zikiendelea kufanywa na vikosi vya uokoaji.

"Miili iliyotolewa eneo la tukio mpaka sasa ni 36 na majeruhi 23 ambao wamekimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu. Zoezi bado linaendelea," amesema Kamanda Mkomagi.

Ajali hiyo imetokea leo jioni katika barabara kuu ya Moshi–Same, ambapo basi la Chanel One lililokuwa likitokea Moshi kuelekea Tanga, liligongana uso kwa uso na Coaster iliyokuwa ikitokea Same kuelekea Moshi.

Taarifa kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa abiria waliokuwemo kwenye Coaster walikuwa wakielekea katika sherehe ya harusi iliyopangwa kufanyika katika ukumbi wa Kuringe Hall, uliopo mjini Moshi.

Jeshi la Polisi na vyombo vya usalama vinaendelea kuchunguza chanzo cha ajali hiyo huku miili ya marehemu ikiendelea kuondolewa kutoka eneo la tukio.

CPA KASORE ASISITIZA UMUHIMU WA KUFUNDISHA MAFUNZO YA UFUNDI STADI KWA WATOTO ILI WAWEZE KUJITEGEMEA

CPA KASORE ASISITIZA UMUHIMU WA KUFUNDISHA MAFUNZO YA UFUNDI STADI KWA WATOTO ILI WAWEZE KUJITEGEMEA

TPDC YAJIVUNIA MAFANIKIO YAPATA TUZO SABASABA.

TPDC YAJIVUNIA MAFANIKIO YAPATA TUZO SABASABA.

TANESCO YATOA MAJIKO YA UMEME KWA WANANCHI SABASABA.

TANESCO YATOA MAJIKO YA UMEME KWA WANANCHI SABASABA.

Waziri Ridhiwani Atoa Wito kwa Vijana Kuchangamkia Fursa Zilizopo.

Waziri Ridhiwani Atoa Wito kwa Vijana Kuchangamkia Fursa Zilizopo.

TPDC ,DC CPP na CPTDC ZASAINI MAKUBALIANO UJENZI WA BOMBA LA GESI ASILIA KUTOKA NTORYA HADI MADIMBA.

TPDC ,DC CPP na CPTDC ZASAINI MAKUBALIANO UJENZI WA BOMBA LA GESI ASILIA KUTOKA NTORYA HADI MADIMBA.