

Lugha ya kiswahili na utamaduni wa mtanzania vimeendelea kuwa kivutio kikubwa kwa wageni mbalimbali wa kimataifa waliotembelea banda la Tanzania katika Wiki ya utamaduni na Kiswahili inayoendelea kwenye maonesho ya biashara ya dunia (Expo 2025) yanayofanyika Osaka.
Viongozi waandamizi wa mataifa mbalimbali, wametembelea banda hilo ikiwemo Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi la Japani, Bw. Koichiro Gemba, Mfalme wa Lesotho, Mhe. Letsie III na Mhe. Prudence Sebahizi, Waziri wa Biashara na Viwanda wa Rwanda.
Viongozi hao wameonesha kuvutiwa kwa kiasi kikubwa na lugha ya Kiswahili na Utamaduni kupata nafasi katika Maonesho hayo ya Dunia yenye hadhi kubwa.
Akizungumza wakati alipotembelea banda hilo Mhe. Sebahizi alieleza kufurahishwa na namna lugha ya Kiswahili ilivyopewa nafasi katika maonesho hayo ya dunia na kudai Kiswahili kinaweza kuwa nyenzo muhimu katika kuwaunganisha Waafrika katika juhudi zao za kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Akizungumza na maofisa wa taasisi za Tanzania zinazoshiriki katika maonesho hayo, ikiwemo Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) na Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA), Mhe. Sebahizi amesema kuwa lugha ya kiswahili inakidhi kwa matumizi miongoni mwa Waafrika
Viongozi hao pia walipata fursa ya kujionea vivutio vya kitamaduni kama vile mavazi ya jadi, sanaa za mikono, bidhaa za kipekee kama kahawa ya Kilimanjaro, Madini ya Tanzanite, viungo vya asili vya Zanzibar na machapisho mbalimbali ya Kiswahili huku Kamusi Kuu ya Kiswahili kutoka BAKITA ikiwavutia wengi.
Ushiriki huu wa Tanzania katika maonesho hayo ambayo kwa upande wa Tanzania yanaratibiwa na TanTrade, ni sehemu ya juhudi endelevu za kuitangaza lugha ya Kiswahili kama urithi wa Afrika na dunia, sambamba na utamaduni wake tajiri, ili kuimarisha uhusiano ya kimataifa na kuvutia wawekezaji, watalii na washirika wa maendeleo kupitia nguvu ya lugha na utambulisho wa kitaifa.
Kilele cha wiki hii ya Utamaduni na Kiswahili katika maonesho hayo kitafanyika tarehe 7 mwezi wa 7, ambapo kwa kawaida huwa ni Maadhimisho ya Siku Kiswahili Duniani (MASIKIDU), ambapo kutakuwa na utoaji wa vyeti na tuzo mbalimbali kwa wadau walioshiriki kwa hali na mali kukikuza, kukieneza, na kukiendeleza Kiswahili nchini Japani.
IDADI YA WATALII WA NDANI WALIOTEMBELEA MKOA WA TABORA IMEONGEZEKA.
DK.NDUMBARO AIPONGEZA OFISI YA MWANDISHI MKUU WA SHERIA.
DKT. YONAZI AONGOZA KIKAO CHA TANZANIA NATIONAL COORDINATING MECHANISM (TNCM)
TANZANIA INA UMEME WA KUTOSHA – DKT. BITEKO
MAMA JANETH MAGUFULI ATEMBELEA BANDA LA OFISI YA WAZIRI MKUU SABASABA*
UDOM KUJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA KUUZA VIMIMINIKA.
Mkoa wa Katavi umeendelea kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM)
SINGIDA YANG'ARA SEKTA YA UTALII.
OFISI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA KUTOA ELIMU YA SHERIA ZA UCHAGUZI SABASABA.
TPDC ,DC CPP na CPTDC ZASAINI MAKUBALIANO UJENZI WA BOMBA LA GESI ASILIA KUTOKA NTORYA HADI MADIMBA.