

Mtangazaji maarufu wa kituo cha redio cha EFM, #DrKumbuka, ametoa kauli kali kuhusu kuvunjika kwa ndoa ya aliyekuwa msemaji wa klabu ya Simba, #HajiManara, na mrembo wake #Zaiylissa.
Akizungumza kwenye kipindi chake, #DrKumbuka amesema kuwa, “Mwanaume kurogwa kwenye mapenzi ni kitu cha kawaida kabisa. Wengine tunarogwa kimapenzi na hatujui.”
Kauli hiyo imekuja baada ya taarifa kusambaa mtandaoni zikionesha kuwa ndoa ya Manara na Zaiylissa imevunjika rasmi, huku wawili hao wakidaiwa kutoleana vitu vya ndani na kuacha nyumba ikiwa tupu.
Katika ushauri wake kwa Haji Manara, Dr Kumbuka alieleza kuwa endapo atahitaji kufunga ndoa tena, ni muhimu kutafuta mwanamke aliyekomaa kiakili, kihisia, na ambaye wanalingana kiumri.
“Ndoa si picha za Instagram, ni maisha halisi. Tafuta mtu ambaye amemaliza kila kitu – siyo bado yupo kwenye kipindi cha kujaribu maisha.” – aliongeza.
Hadi sasa, Manara hajatoa kauli rasmi kuhusu kilichojiri, lakini mashabiki wake mitandaoni wameendelea kumshauri apumzike kwanza kabla ya kurudi tena kwenye anga za mapenzi.
PPAA yatoa elimu matumizi ya Moduli Wiki ya Utumishi wa Umma
KIHENZILE: UWAZI NA UWAJIBIKAJI NI NGUZO MUHIMU ZENYE TIJA KWA WANANCHI
KIHENZILE:WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NI FURSA MUHIMU KWA WANANCHI
ACT WAZALENDO KUUWASHA MOTO MANZESE WAJIDHATITI KUCHUKUA MAJIMBO YOTE DAR ES SALAAM
TANESCO YAJA NA KAMPENI MAALUM YA KUHAMASISHA ULIPAJI WA MADENI KWA WATEJA.
GRAND BUNGE BONANZA KUFANYIKA JUNI 21 2025 HUKU MGENI RASMI AKITARAJIWA KUWA RAIS SAMIA.
KIHENZILE:WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NI FURSA MUHIMU KWA WANANCHI
NISHATI YA GESI ASILIA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA NCHI.
MOI YASEMA WAGONJWA WENGI WANAOWAHUDUMIA WANA MATATIZO SUGU.
CDE SALUM ATANGAZA NIA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KAHAMA MJINI.