NISHATI YA GESI ASILIA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA NCHI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Nishati

NISHATI YA GESI ASILIA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA NCHI.

Nishati ya gesi asilia imekuwa na Mchango mkubwa Kwa nchi hasa kwenye Sekta ya umeme ambapo Serikali imewekeza kwenye bwawa la umeme hii ni nishati muhimu

Moreen Rojas, Dodoma
By Moreen Rojas, Dodoma
17 Jun 2025
NISHATI YA GESI ASILIA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA NCHI.

Nasasa gesi hii ni muhimu Kwa Matumizi ya majumbani viwandani na magari nasasa upo mpango gesi hii itumike zaidi kwenye magari na maeneo mengine ya nchi Kwa gesi hiyo imekuwa ikipatika Mtwara Lindi na Dar es salam

Hayo yameelezwa Leo na Charles Nyangi Mkuu wa kitengo cha ushirikishwaji wa wazawa na ushirikishwaji wa ndani kutoka Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ufunguzi wa Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2025 yaliyofanyika katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

Ameongeza kuwa gesi hii itafika katika mikoa mingine kadri wananchi watakavyoielewa na kuona umuhimu wake Kwa kurahisisha na kuhimiza  Matumizi ya nishati safi.

Aidha amesema Wapo kwenye Maonesho hayo kuwaelezea Wananchi kuhusu shughuli zinazofanywa na Mamlaka hiyo pamoja na fursa zinazokuwepo katika shughuli za Mkondo wa juu wa Petroli

PURA ilianzishwa chini ya Sheria ya Petroli mwaka 2015  na moja la jukumu lilipoewa ni kuhamasisha ushiriki wa wawazawa katoka shughuli za Mkondo wa juu wa Petroli.

Amesema ushiriki huo umegawanywa katikati makundi matatu ambayo ni Kupitia ajira,kupitia ujasiriamali kwa maana ya  kununua na kusambaza Bidhaa au uwekezaji.

" Hivyo tunapokuwa katika Maonesho haya ni kuwaelezea Wananchi majukumu na shughuli zinazopatikana kwenye mkono ," amesema

PURA ina matumaini kuwa ifikapo mwishoni mwa mwaka huu, wawekezaji watakuwa wamepatikana, jambo ambalo litaleta manufaa kwa wananchi na taifa kwa ujumla.

Sanjari na hayo PURA inafanya kazi ya Kuwajengea uwezo watanzania na kampuni za Kitanzania kushiriki kikamilifu katika miradi ya utafutaji,uendelezaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia pamoja na kuhamasisha uwekezaji katika shughuli za mafuta na gesi asilia nchini.

Maadhimisho hayo yamebeba kauli mbiu isemayo "Himiza Matumizi ya mifumo ya kidijiti ili kuongeza upatikanaji wa taarifa na kuchagiza uwajibikaji"

REA Yashukuru Maono ya Rais Samia, Yajipanga Kusambaza Umeme na Nishati Safi Hadi Vitongojini

REA Yashukuru Maono ya Rais Samia, Yajipanga Kusambaza Umeme na Nishati Safi Hadi Vitongojini

EWURA YABORESHA UPATIKANAJI WA HUDUMA KWENYE MITANDAO YAO YA KIJAMII

EWURA YABORESHA UPATIKANAJI WA HUDUMA KWENYE MITANDAO YAO YA KIJAMII

DKT. BITEKO AZINDUA MKAKATI WA TAIFA WA MAWASILIANO WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

DKT. BITEKO AZINDUA MKAKATI WA TAIFA WA MAWASILIANO WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

Morocco wampongeza Rais Samia kwa usimamizi bora Sekta ya Nishati

Morocco wampongeza Rais Samia kwa usimamizi bora Sekta ya Nishati

Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.

Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.