

Mwandishi Mkuu wa Sheria, Onorius Njole amesema toleo la Sheria ambazo zimetafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili zinatarajiwa kuanza kutoka ifikapo Agosti mwaka huu ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuagiza kutafsiriwa kwa sheria ili iweze kueleweka kwa urahisi na watu wa makundi yote.
Mwandishi Mkuu wa Sheria, Onorius Njole amesema toleo la Sheria ambazo zimetafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili zinatarajiwa kuanza kutoka ifikapo Agosti mwaka huu ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuagiza kutafsiriwa kwa sheria ili iweze kueleweka kwa urahisi na watu wa makundi yote.
Hayo ameyasema leo Julai 6, 2025 jijini Dar es salaam kwenye maonesho ya 49 ya kimataifa ya biashara mara baada ya kutembelea banda Mwandishi Mkuu wa Sheria lililopo kwenye maonesho hayo ya sabasaba.
Amesema kuwa sambamba na kuendelea na mchakato wa kukamilisha zoezi hilo pia Ofisi hiyo imefanya mabadiliko makubwa ya kuhakikisha sheria zilizopo zinatekelezeka na kuwafikia wananchi.
“Mpaka sasa tumefanya mabadiliko makubwa ya kuhakikisha tunakuwa na sheria zinazowafikia wananchi kama Sheria na ukamilifu wake na lugha ambayo wananchi wanaifahamu” amesema Njole.
Ameongeza kuwa ofisi hiyo imefanya urekebu wa sheria mbalimbali ili ziweze kuendana na mahitaji ya sasa ya nchi “ tumefanya urekebu wa Sheria hizi kwa kuzikisanya sheria zote za nchi pamoja na kuingiza marekebisho ambayo yamekuwa yakifanyika kila wakati” amesema
Pamoja na hayo, amesema kuwa Serikali ipo katika mchakato wa kutengeneza mfumo wa sheria wa kusimamia matumizi ya Akili Mnemba (IA) na kubainisha kuwa mchakato huo utakapokuwa tayari utaandaliwa sheria.
Kwa upande wake Mwandishi Mkuu Msaidizi wa Sheria, Rehema Katuga amesema kuwa baada ya kukamilika kwa urekebu wa sheria mbalimbali ambazo zimeanza kutumika Julai mosi mwaka huu za awali hazitatumika tena.
IDADI YA WATALII WA NDANI WALIOTEMBELEA MKOA WA TABORA IMEONGEZEKA.
DK.NDUMBARO AIPONGEZA OFISI YA MWANDISHI MKUU WA SHERIA.
DKT. YONAZI AONGOZA KIKAO CHA TANZANIA NATIONAL COORDINATING MECHANISM (TNCM)
TANZANIA INA UMEME WA KUTOSHA – DKT. BITEKO
MAMA JANETH MAGUFULI ATEMBELEA BANDA LA OFISI YA WAZIRI MKUU SABASABA*
UDOM KUJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA KUUZA VIMIMINIKA.
Mkoa wa Katavi umeendelea kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM)
SINGIDA YANG'ARA SEKTA YA UTALII.
TANZANIA YAENDELEA KUTANGAZA NA KUKUZA KISWAHILI NA UTAMADUNI WAKE KIMATAIFA
OFISI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA KUTOA ELIMU YA SHERIA ZA UCHAGUZI SABASABA.