Mashindano ya Polisi Jamii Kuimarisha mahusiano kati ya Polisi na Wananchi | The Dodoma Post
The Dodoma Post Michezo

Mashindano ya Polisi Jamii Kuimarisha mahusiano kati ya Polisi na Wananchi

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) George Katabazi, alisema kuwa mashindano ya Polisi Jamii Umoja Cup yamehusisha jumla ya timu 14 kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa huo, kwa lengo la kuimarisha mahusiano kati ya Jeshi la Polisi na wananchi.

Moreen Rojas
By Moreen Rojas
20 May 2025
Mashindano ya Polisi Jamii  Kuimarisha mahusiano kati ya Polisi na Wananchi

Akizungumza wakati wa fainali ya Polisi Jamii Cup kati ya timu ya Mpunguzi na Chang’ombe, Katabazi alisema mashindano hayo si tu burudani bali pia ni chombo cha malezi ya uzalendo, nidhamu na ushiriki wa kijamii.

Alibainisha kuwa kupitia mashindano hayo, Jeshi la Polisi linakusudia kujenga uelewa na ushirikiano wa karibu na jamii ili kuhakikisha wanajiepusha na vitendo vya kihalifu pamoja na kushiriki kikamilifu katika utoaji wa taarifa kuhusu uhalifu na wahalifu.

“Tunatumia michezo kama jukwaa la kuleta mshikamano, kuwahamasisha vijana kuepuka uhalifu na kuwa sehemu ya suluhisho kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kulinda amani ya maeneo yao,” alisema ACP Katabazi.

Kwa upande wake MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, amesema michezo inaweza kuwa daraja muhimu la kuwahamasisha vijana kushiriki katika mchakato wa kidemokrasia, hususan kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

“Michezo siyo tu ushindani wa uwanjani. Ni darasa la maisha. Hapa vijana wanajifunza mshikamano, uvumilivu, na uzalendo—nguzo kuu za uchaguzi wa amani,” alisema RC Senyamule.

Aliongeza kuwa Serikali ya Mkoa wa Dodoma itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kutumia michezo kama jukwaa la kutoa elimu ya uraia, kuhimiza usalama wa jamii na kuhamasisha vijana kujitokeza kujiandikisha na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi.

“Rais Samia ameendelea kuwekeza kwa vijana kupitia michezo na programu mbalimbali. Tunapowaona vijana wakijitokeza kama hawa wa Polisi Jamii Cup, tunaona picha ya Taifa lenye matumaini,” alisema.

Aidha, aliwasihi vijana kutumia nafasi ya sasa sio tu kujiandikisha kama wapiga kura bali pia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, huku akisisitiza umuhimu wa kuepuka kauli na vitendo vinavyoweza kuvuruga amani.

GRAND BUNGE  BONANZA KUFANYIKA  JUNI 21 2025 HUKU MGENI RASMI AKITARAJIWA KUWA RAIS SAMIA.

GRAND BUNGE BONANZA KUFANYIKA JUNI 21 2025 HUKU MGENI RASMI AKITARAJIWA KUWA RAIS SAMIA.

DODOMA YAELEKEA IRINGA KWA KISHINDO MASHINDANO YA UMISSETA.

DODOMA YAELEKEA IRINGA KWA KISHINDO MASHINDANO YA UMISSETA.

Simba SC Yajivunia Kuendelea na Vita Baada ya Kudondosha Pointi Moroco

Simba SC Yajivunia Kuendelea na Vita Baada ya Kudondosha Pointi Moroco

ALLY KAMWE mikononi mwa Polisi, yataja chanzo

ALLY KAMWE mikononi mwa Polisi, yataja chanzo

Wazee wa Yanga Dodoma watoa msimamo wataka Karia aombe radhi

Wazee wa Yanga Dodoma watoa msimamo wataka Karia aombe radhi