

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maono yake makubwa yaliyochangia kwa kiasi kikubwa kuifikia jamii ya vijijini kupitia upatikanaji wa nishati ya umeme na kuchochea kampeni ya matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.
Akizungumza katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Utawala wa REA, Bw. Renatus Msangira, alisema kuwa juhudi za Rais Samia zimewezesha kufikiwa kwa vijiji vyote nchini kupitia huduma ya umeme, na sasa wakala unaelekeza nguvu zake katika kusambaza huduma hiyo hadi kwenye vitongoji.
“Kwa niaba ya Bodi ya Wakurugenzi wa REA, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa maono yake. Kupitia dira yake, tumefanikisha kupeleka umeme katika vijiji vyote nchini, na sasa tumeanza awamu mpya ya kuhakikisha vitongoji vyote navyo vinaunganishwa na huduma hiyo muhimu,” alisema Msangira.
Aidha, alieleza kuwa REA inaunga mkono kwa vitendo kaulimbiu ya Rais Samia inayosisitiza matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa afya na mazingira bora. Alisema wakala umeanza kusambaza majiko ya umeme yenye matumizi nafuu, likiwemo jiko linalotumia uniti moja tu ya umeme kwa saa moja.
“Hii ni sehemu ya kampeni ya matumizi ya nishati safi. Kwa sasa tumeanza na taasisi za umma, hasa zile zinazotoa huduma kwa watu zaidi ya 100, kama vile shule na hospitali, na tutaendelea kuwafikia wananchi wengine kote nchini,” alibainisha.
Bw. Msangira aliwataka wananchi kufika kwenye banda la REA katika viwanja vya maonesho Dodoma ili kujionea miradi inayotekelezwa na wakala huo, sambamba na kupata elimu kuhusu huduma za umeme vijijini na matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanawakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya umma kutoa huduma moja kwa moja kwa wananchi, kueleza majukumu yao na kutoa mrejesho wa maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya serikali.
PPAA yatoa elimu matumizi ya Moduli Wiki ya Utumishi wa Umma
KIHENZILE: UWAZI NA UWAJIBIKAJI NI NGUZO MUHIMU ZENYE TIJA KWA WANANCHI
KIHENZILE:WIKI YA UTUMISHI WA UMMA NI FURSA MUHIMU KWA WANANCHI
ACT WAZALENDO KUUWASHA MOTO MANZESE WAJIDHATITI KUCHUKUA MAJIMBO YOTE DAR ES SALAAM
TANESCO YAJA NA KAMPENI MAALUM YA KUHAMASISHA ULIPAJI WA MADENI KWA WATEJA.
DODOMA YAELEKEA IRINGA KWA KISHINDO MASHINDANO YA UMISSETA.
Serikali Yatangaza Kuanza Msako Kuwabaini Wanaotumikisha Watoto
GRAND BUNGE BONANZA KUFANYIKA JUNI 21 2025 HUKU MGENI RASMI AKITARAJIWA KUWA RAIS SAMIA.
MOI YASEMA WAGONJWA WENGI WANAOWAHUDUMIA WANA MATATIZO SUGU.
NISHATI YA GESI ASILIA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA NCHI.