REA Yashukuru Maono ya Rais Samia, Yajipanga Kusambaza Umeme na Nishati Safi Hadi Vitongojini | The Dodoma Post
The Dodoma Post Nishati

REA Yashukuru Maono ya Rais Samia, Yajipanga Kusambaza Umeme na Nishati Safi Hadi Vitongojini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maono yake makubwa yaliyochangia kwa kiasi kikubwa kuifikia jamii ya vijijini kupitia upatikanaji wa nishati ya umeme na kuchochea kampeni ya matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Moreen Rojas, Dodoma
By Moreen Rojas, Dodoma
17 Jun 2025
REA Yashukuru Maono ya Rais Samia, Yajipanga Kusambaza Umeme na Nishati Safi Hadi Vitongojini

Akizungumza katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Utawala wa REA, Bw. Renatus Msangira, alisema kuwa juhudi za Rais Samia zimewezesha kufikiwa kwa vijiji vyote nchini kupitia huduma ya umeme, na sasa wakala unaelekeza nguvu zake katika kusambaza huduma hiyo hadi kwenye vitongoji.

“Kwa niaba ya Bodi ya Wakurugenzi wa REA, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa maono yake. Kupitia dira yake, tumefanikisha kupeleka umeme katika vijiji vyote nchini, na sasa tumeanza awamu mpya ya kuhakikisha vitongoji vyote navyo vinaunganishwa na huduma hiyo muhimu,” alisema Msangira.

Aidha, alieleza kuwa REA inaunga mkono kwa vitendo kaulimbiu ya Rais Samia inayosisitiza matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa afya na mazingira bora. Alisema wakala umeanza kusambaza majiko ya umeme yenye matumizi nafuu, likiwemo jiko linalotumia uniti moja tu ya umeme kwa saa moja.

“Hii ni sehemu ya kampeni ya matumizi ya nishati safi. Kwa sasa tumeanza na taasisi za umma, hasa zile zinazotoa huduma kwa watu zaidi ya 100, kama vile shule na hospitali, na tutaendelea kuwafikia wananchi wengine kote nchini,” alibainisha.

Bw. Msangira aliwataka wananchi kufika kwenye banda la REA katika viwanja vya maonesho Dodoma ili kujionea miradi inayotekelezwa na wakala huo, sambamba na kupata elimu kuhusu huduma za umeme vijijini na matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanawakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya umma kutoa huduma moja kwa moja kwa wananchi, kueleza majukumu yao na kutoa mrejesho wa maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya serikali.

EWURA YABORESHA UPATIKANAJI WA HUDUMA KWENYE MITANDAO YAO YA KIJAMII

EWURA YABORESHA UPATIKANAJI WA HUDUMA KWENYE MITANDAO YAO YA KIJAMII

NISHATI YA GESI ASILIA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA NCHI.

NISHATI YA GESI ASILIA IMEKUWA NA MCHANGO MKUBWA KWA NCHI.

DKT. BITEKO AZINDUA MKAKATI WA TAIFA WA MAWASILIANO WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

DKT. BITEKO AZINDUA MKAKATI WA TAIFA WA MAWASILIANO WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA.

Morocco wampongeza Rais Samia kwa usimamizi bora Sekta ya Nishati

Morocco wampongeza Rais Samia kwa usimamizi bora Sekta ya Nishati

Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.

Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.