BRELA yatoa Gawio la Shilingi Bilioni 20.4 kwa Serikali | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

BRELA yatoa Gawio la Shilingi Bilioni 20.4 kwa Serikali

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imetoa gawio la Shilingi Bilioni 20.4 kwa Serikali kwa mwaka 2025, likiwa ni ongezeko kutoka Shilingi Bilioni 18.9 zilizotolewa mwaka 2024.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
10 Jun 2025
BRELA yatoa Gawio la Shilingi Bilioni 20.4 kwa Serikali

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imetoa gawio la Shilingi Bilioni 20.4 kwa Serikali kwa mwaka 2025, likiwa ni ongezeko kutoka Shilingi Bilioni 18.9 zilizotolewa mwaka 2024.

Gawio hilo limetolewa leo JUNE 10, Ikulu jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika hafla ya kupokea gawio na michango kutoka kwa taasisi na mashirika ya umma.

Vilevile, BRELA imepokea tuzo kama Taasisi iliyofanya vizuri katika kuchangia gawio kila mwaka, kwa wastani wa Shilingi Bilioni 16.8 kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo.

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na taasisi husika, wakiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya BRELA, Prof. Neema Mori, pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa.

TANESCO YAJA NA KAMPENI MAALUM YA KUHAMASISHA ULIPAJI WA MADENI KWA WATEJA.

TANESCO YAJA NA KAMPENI MAALUM YA KUHAMASISHA ULIPAJI WA MADENI KWA WATEJA.

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 107 ZAKAMILISHA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI SIMIYU

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 107 ZAKAMILISHA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI SIMIYU

MEATU MTAENDELEA KUPATA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO IKIWEMO NISHATI- DKT.SAMIA

MEATU MTAENDELEA KUPATA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO IKIWEMO NISHATI- DKT.SAMIA

Mifumo Ya Kidijitali Yaleta Mageuzi Makubwa Katika Sekta Ya Umma:Simbachawene

Mifumo Ya Kidijitali Yaleta Mageuzi Makubwa Katika Sekta Ya Umma:Simbachawene

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA.

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA.